Wednesday, 17 May 2017

Kiongozi wa zamani wa FBI kuchunguza iwapo Urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani Saa moja iliyopita Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpya Sambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii Twitter Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Email Mshirikishe mwenzako


Robert Mueller aliingoza FBI kuanzia 2001 - 2013Wizara ya sheria nchini Marekani, imetangaza kuteuliwa kwa mwendesha mashtaka maalum atakae ongoza uchuguzi wa tuhuma kwamba Urusi iliingilia uchaguzi wa marekani wa mwaka jana.
Mwendesha mashtaka huyo aliwahi kuwa mkuu wa shirika la kijajusi la FBI, Robert Mueller.
Pia katika uchunguzi wake, atazingatia iwapo kulikuwa na mwingiliano wa aina yoyote kati ya Urusi na timu ya kampeni ya Trump.
Taarifa iliyotolewa na wizara ya sheria nchini humo imesema uchunguzi huo utaongozwa na mtu asiyeegemea upande wowote kwa ajili ya maslahi ya umma.
Tangazo hilo linafuatia utata uliogubikwa kufuatia kufutwa kazi kwa wiki moja iliyopita kwa James Comey, ambae ndie aliyekuwa akiongoza uchunguzi huo.

No comments:

Post a Comment